Skip to main content

Biashara

Biashara

Kuwezesha ukuaji wa sekta ya kilimo kupitia huduma mahususi za fedha

TADB inatoa huduma za fedha zilizobuniwa kukidhi mahitaji mbalimbali ya sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi nchini Tanzania.

Mikopo yetu imegawanyika katika makundi makuu mawili ambayo ni (i)Mikopo ya Moja kwa Moja inayowaruhusu wateja kukopa moja kwa moja kutoka TADB kupitia huduma mbalimbali za fedha na (ii) Mikopo isiyo ya Moja kwa Moja inayowaruhusu wateja kukopeshwa na TADB kupitia taasisi shiriki za fedha. Aidha, huduma za mikopo zinazotolewa kwa njia isiyo ya moja kwa moja ni pamoja na mfuko wa dhamana wa wakulima wadogo; na mikopo ya jumla kwa taasisi za fedha.

Bidhaa zenye mnyororo wa thamani

Bidhaa

Kama mteja wetu wa thamani, unakuletewa bidhaa bunifu zinazobadilisha urahisi wa huduma za kibenki. Kwa utaalamu wetu, unaweza kuwa na uhakika kwamba mradi wako unalindwa na kulelewa kwa wakati mmoja.

''Kuongeza Tija Katika uzalishaji '' Upatikanaji wa zana za kisasa zinazohitajika kuongeza ufanisi na kutanua wigo wa uzalishaji.
"Kuwezesha Viwanda vya Mazao ya Kilimo" Kutoa mikopo ya muda mrefu kwa ajili ya kuwezesha ujenzi wa miundombinu ya miradi ya uchakataji wa mazao itakayochochea ukuaji wa sekta ya kilimo nchini.
"Kuwezesha upatikanaji wa mitaji katika msimu husika" ili kurahisisha utendaji kazi katika hatua mbalimbali za mnyororo wa thamani kuanzia kupanda hadi kuuza kwa mlaji wa mwisho.
Kuwezesha upatikanaji wa mikopo kwa wakulima wadogo kupitia dhamana inayotolewa kwa taasisi za fedha shiriki.