Skip to main content

Mikopo ya miundombinu ya uzalishaji

Hii inalenga kufadhili ununuzi wa mali kwa ajili ya kuwezesha matumizi ya mashine katika kilimo, yaani matrekta, mashine za kuvuna, mashine za kupanda, vifaa vya umwagiliaji, mashine na vifaa vya kuongeza thamani ya mazao, vifaa/teknolojia ya usimamizi wa mazao baada ya mavuno, na mahitaji mengine ya ufadhili wa mali yanayokusudiwa kuongeza uzalishaji, kuongeza thamani na masoko.

Mkopo unalipwa kulingana na mpango wa malipo, mtiririko wa fedha wa mradi, na aina ya mkopo, yaani mkopo wa muda mfupi, mkopo wa muda wa kati au mkopo wa muda mrefu. Malipo ya mkopo hufanyika kwa awamu na kwa kuzingatia kipindi cha kurejesha mkopo.

LENGO LA MKOPO

Kufadhili shughuli za kabla na baada ya mavuno (yaani maandalizi ya shamba, ununuzi wa pembejeo, matunzo na uvunaji), ununuzi wa wanyama (kama vile mifugo, kuku, vifaranga vya samaki).

SOKO LENGWA

Wakulima Wadogo (SHF), Taasisi, Wajasiriamali Wadogo na wa Kati (SME), Wafugaji, Wakusanyaji Mazao, Taasisi za Uvuvi, na Vyama vya Kusaidiana (ROSCAs).

KIWANGO CHA MKOPO

Kiasi cha mkopo wa muda maalum hakipaswi kuzidi asilimia 75 ya gharama za mradi.

Kumbuka: Mikopo yote ya muda maalum itategemea uhalisia na uwezo wa mradi kulingana na pendekezo la biashara ya kifedha litakalowasilishwa na mkopaji.

MASHARTI YA ULIPAJI

Kulipwa kwa awamu (kila mwezi, kila robo mwaka au kila nusu mwaka) ikijumuisha mtaji na riba, kulingana na mapato halisi ya mtiririko wa fedha.

KIPINDI CHA MSAMAHA

Isizidi mwaka 1

MUDA WA KUKAMILISHA

Mwaka 1