Kuhusu Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ni taasisi ya kifedha ya maendeleo, iliyoanzishwa chini ya sheria ya makampuni ya mwaka 2002 kisha kusajiliwa chini ya sheria ya mabenki na taasisi za fedha Na. 5 ya mwaka 2006 kwa lengo la kutoa mikopo ya muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu ili kuleta mapinduzi ya sekta ya kilimo nchini Tanzania.
Tunu za Msingi
- Uadilifu – Kudumisha uwazi, uwajibikaji, na viwango vya juu vya maadili.
- Kujifunza na Ubunifu - Kuchochea ubunifu endelevu na imara.
- Weledi - Kufanya kazi kwa kuzingatia ujuzi, maarifa, na viwango vya kitaalamu.
- Kufanya kazi kama timu - Kushirikiana kwa ufanisi ili kufikia malengo ya pamoja.
- Mitizamo Tofauti na Ushirikishwaji - Kuheshimu na kuthamini mawazo, mitizamo na ushiriki wa watu wote.
Malengo Makuu
- Kuchangia katika utoshelevu na usalama wa chakula.
- Kuleta mapinduzi ya kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda kilimo cha kibiashara kitakachochangia ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini.