Skip to main content

Mikopo kwa ajili ya miradi ya kimkakati

Huu ni ufadhili wa muda mrefu wa miundombinu na miradi ya viwanda unaotegemea makadirio ya mtiririko wa fedha wa mradi pamoja na Taarifa za Kifedha za awali za mdhamini.

Unakusudiwa kufadhili mahitaji ya miundombinu ya mnyororo wa thamani wa kilimo kama vile ujenzi wa miradi ya umwagiliaji, maghala ya kisasa ya kuhifadhia mazao, vituo vya masoko na mahitaji mengine ya mikopo ya miundombinu ya kilimo kwa ajili ya kujenga na kuimarisha minyororo ya thamani ya kilimo. Mkopo unalipwa kulingana na mpango wa malipo, mtiririko wa fedha wa mradi, na kulingana na aina ya mkopo kama vile mkopo wa muda mfupi, mkopo wa muda wa kati au mkopo wa muda mrefu. Ulipaji wa mkopo unafanyika kwa awamu na kwa kuzingatia muda wa kurejesha mkopo.

LENGO LA MKOPO

Kufadhili shughuli za kabla na baada ya mavuno (yaani maandalizi ya shamba, ununuzi wa pembejeo, matunzo na uvunaji), ununuzi wa wanyama (kama vile mifugo, kuku, vifaranga vya samaki).

SOKO LENGWA

Wakulima Wadogo, Taasisi, Wajasiriamali Wadogo na wa Kati, Wafugaji, Wakusanyaji mazao, Taasisi za Uvuvi.

KIWANGO CHA MKOPO

Kiasi cha mkopo wa muda maalum hakipaswi kuzidi asilimia 75 ya gharama za mradi.

Kumbuka: Mikopo yote ya muda maalum itategemea uhalisia na uwezo wa mradi kulingana na pendekezo la biashara ya kifedha litakalowasilishwa na mkopaji.

MASHARTI YA ULIPAJI

Kulipwa kwa awamu (kila mwezi, kila robo mwaka au kila nusu mwaka) ikijumuisha mtaji na riba, kulingana na mapato halisi ya mtiririko wa fedha.

KIPINDI CHA MSAMAHA

Isizidi miaka 2

MUDA WA KUKAMILISHA

Miaka 1-15