Serikali inaelekeza TADB kupunguza viwango vya riba

Serikali yaiagiza TADB kupunguza riba kutoka asilimia 11 hadi 9 kwa wakulima wa kahawa mkoani Kagera, hii itasaidia kupunguza gharama za mkopo na kuongeza tija.

Maagizo hayo yalitolewa jana na Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe alipokuwa akizungumza na viongozi kutoka mikoa inayolima kahawa nchini.Bashe alisema lengo la kuitaka TADB kupunguza riba ni kuwasaidia wakulima kuendesha kilimo cha kahawa kwa faida.

Chanzo - IPP Media