
TADB imeendesha mafunzo ya siku nane kwa wakulima wa michikichi wilayani Kigoma yenye lengo la kukuza uelewa wa chapa na huduma, kuwajengea uwezo katika elimu ya biashara, fedha na usimamizi wa mikopo ya mikopo, pamoja na kuwafundisha kanuni bora za uzalishaji katika kilimo.

Kigoma ni Mkoa wa Tanzania unaozalisha michikichi kwa wingi ambapo jumla ya hekta 2,877.5 za wakulima hao wamepata mikopo yenye masharti nafuu ili kuwezesha na kulainisha uendeshaji wa miradi ya michikichi na kuweza kuzalisha kwa wingi ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

KATIKA KUWEZESHA MTANDAO WA THAMANI WA KILIMO CHA MAWESE, TADB TAYARI IMEIDHINISHA MIKOPO YA WAKULIMA WA MAWESE ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1.9.
Zaidi ya wanachama 1,044 wa AMCOS (wanawake 218, vijana 313 na wanaume 513) wanufaika wa mikopo ya TADB mkoani Kigoma.
